WALALA MBELE WAKIHOFIA KUKAMATWA NA TANESCO

 
Moshi

WAKAZI wa Kibosho Manushi kata ya Kindi mkoani Kilimanjaro wamelazimika kukimbia makazi yao kwa kuogopa kamatakamata ya wa polisi maofisa wa shirika la umeme Tanesco kutokana na wakazi hao kujiingizi umeme kinyume cha sheria. 

Kaimu meneja wa shirika la Tanesco Honest Moshi, alisema hayo jana  wakati walipotembelea nyumba za watu wakazi wa kibosho Manushi  ambao wanajiingizia umeme majumba kwa kutoka kwenye nguzo za umeme.

Moshi alisema katika nyumba 15 walizotembelea walikuta kuna umeme  ambao umeingizwa kinyemela na kukuta hakuna mtu yoyote katika nyumba hizo

Kaimu  huyo alisema kuwa kibosho  ndiko kulikokithiri kwa wizi wa umeme ambapo nyumba moja inaweza kugawia umeme  nyumba nyingine tano kwa kutumia nyaya nyembamba  hali ambayo ni hatari kwa wakazi hao.

“Taarifa za watu hao tunazo na tutafauatilia mmoja hadi mwingine ili kuweza  kuwakamata wote waliokimbia na kuwafikisha katika vyomba vya sheria”alisema Moshi

Alisema pamoja na wakazi hao kukimbia wamefanikiwa kukamata watu wawili na kuweza kuwafungulia mashata ya kuhujumu shirika hilo.

Kaimu huyo aliwataka wakazi wa kibosho  kuendelea kutoa taarifa za watu wanaotumia umeme kinyume na taratibu za shirika hilo ili waweze kutiwa mbaroni.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo