POLISI WAOKOENI MADEREVA BODA BODA

SIHA
 
MADEREVA wa bodaboda wilayani Siha mkoani Kilimanjaro wamelitaka jeshi la
polisi mkoani hapa kuwachukulia hatua wale wote wanaohusika na matukio ya
utekaji nyara  wa madereva hao ikiwa ni pamoja na kuuwawa kikatili na
kuporwa mali zao  jambo ambalo limekuwa likiwakatisha tama kufanya kazi
hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa mafunzo ya waendesha bodaboda
juu ya kufuta sheria za barabarani ili kuepuka ajili zisizo za lazima,
walisema kuwa kumekuwa na matukio mengi ya utekwaji nyara madereva wa
bodaboda na kuuwawa kikatili kisha kutelekezwa maporini na kupotea katika
mazingira ya kutatanisha.

Walisema jeshi la polisi halina budi kuhakikisha wanaendesha msako mkali

ili kuwabaini watu hao ambao wamekuwa wakifanya vitendo hiyo vya ukiukwaji wa haki za binadamu kutokana na kwamba vijana wengi wamekuwa wakitegemea kazi hiyo ili kujikwamua kutoka katika vimbi la umasini.

Wakizungumza madereva hao Hamisi Shaban na John Masoy, walisema kuwa

kutokana na ukosefu wa ajira nchini vijana wameamua kuingia katika bishara
hiyo na kuondokana na makundi uvutaji wa madawa ya kulevya pamoja na
makundi ya ujambazi na kwamba pasipo kuchukuliwa hatua za hara za kuthibiti tatizo hilo kuna uwezekano mkubwa wa vijana kurudi katika makundi hao.

Aidha madereva hao wameilalamikia halimashauri hiyo kupandisha gharama za

ushuru hadi kufikia kisia cha shilingi 30,000 kwa mwaka jambo ambalo
walisema ni uonevu kutokana na faida ndogo wanayo ipata kutokana na
biashara hiyo kutokana na kuwepo kwa malipo mengi.

Akijibu malalamiko hayo afisa biasara wa wilaya hiyo Christa Ndosa, alisema

kuwa ushuru huo uliwekwa kwa taratibu na sheria za halmashauri hiyo hivyo
ni vyema wakavumilia ushuru huo mpaka hapo sheria hiyo itakapo fanyiwa
marekebisho.
Kwa upande wake mkuu wa makosa ya usalama barabarani Peter Sima aliwataka madereva hao kutoa taarifa haraka polisi ikiwa dereva amemtilia shaka abiria liye mpaki katika pikipiki yake ili kuweza kutia mbaro watekaji wa
pikipiki na wauwaji wa madereva hao.

Aidha aliwataka madereva hao kuhakikisha kuwa wanazingatia sheria za
barabarani ikiwa ni pamoja na kuwa na leseni zinazo waruhusu kufanya
biashara hiyo na leseni ya kuendesha chombo hicho jambo ambalo litapunguza
ajali za mara kwa mara.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo