MAKETE
Wamiliki wa vyombo vya moto wilayani Makete wametakiwa kufuata taratibu zote za umiliki wa vyombo hivyo ili kuondokana na usumbufu usio wa maana pamoja na kuepuka ajali zisizo za lazima
Hayo yamesemwa na Meneja wa mamlaka ya mapato TRA wilaya ya Makete Halid Kimolo katika kiako cha wamiliki wa vyombo vya moto kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Makete kikiwa na lengo la elimu ya umiliki wa vyombo hivyo na utoaji wa leseni
Bw. Kimolo amesema wamiliki wote wanatakiwa kuzingatia vitu vya muhimu kama vile leseni ya chombo chake, kadi pamoja na uendeshaji salama kuongeza kuwa leseni inatakiwa kuwa na majina matatu ya mmiliki wa chombo hicho
Amesema kama kuna mtu anatilia shaka uhalali wa nyaraka za chombo cha usafiri anatakiwa kufika mamlaka ya mapato wilayani hapo kujiridhisha zaidi ili kupata uhakika
Amewataka wamiliki wa vyombo hivyo kutobadilisha majina yao kwani kwa kufanya hivyo kunasababisha usumbufu katika utendaji kazi
Na Kumbuka Kilando & Raphael Abel
Wamiliki wa vyombo vya moto wilayani Makete wametakiwa kufuata taratibu zote za umiliki wa vyombo hivyo ili kuondokana na usumbufu usio wa maana pamoja na kuepuka ajali zisizo za lazima
Hayo yamesemwa na Meneja wa mamlaka ya mapato TRA wilaya ya Makete Halid Kimolo katika kiako cha wamiliki wa vyombo vya moto kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Makete kikiwa na lengo la elimu ya umiliki wa vyombo hivyo na utoaji wa leseni
Bw. Kimolo amesema wamiliki wote wanatakiwa kuzingatia vitu vya muhimu kama vile leseni ya chombo chake, kadi pamoja na uendeshaji salama kuongeza kuwa leseni inatakiwa kuwa na majina matatu ya mmiliki wa chombo hicho
Amesema kama kuna mtu anatilia shaka uhalali wa nyaraka za chombo cha usafiri anatakiwa kufika mamlaka ya mapato wilayani hapo kujiridhisha zaidi ili kupata uhakika
Amewataka wamiliki wa vyombo hivyo kutobadilisha majina yao kwani kwa kufanya hivyo kunasababisha usumbufu katika utendaji kazi
Na Kumbuka Kilando & Raphael Abel