WAKIMBIZI 22 WA KISOMALI WAZIKWA MOROGORO

Na Global Publishers

 
Miili ya wakimbizi hao ikiteremshwa katika makaburi ya Kolla kutoka kwenye lori.
 
Kiongozi wa dini ya Kikrsto akishiriki mazishi hayo.
 
Kiongozi wa dini ya Kiislam aliyeshiriki mazishi hayo.
 
Mwili ukiwa kaburini.
 
Mwili ukitayarishwa kuteremsha kaburini.
 
Mazishi yakiendelea.

WAKIMBIZI kutoka Somalia zaidi ya 100 waliokuwa wakisafiri kwa kificho  kutoka  Ethiopia kwenda nchi za Malawi na Afrika Kusini kwa lengo la kusaka maisha bora baadhi yao walipoteza maisha hivi majuzi  baada ya kukosa hewa wakati wakisafirishwa kwenye kontena ili kuwakwepa maofisa wa Idara ya Uhamiaji nchini.

Tukio hilo lilitokea katikati ya wiki hii mkoani Dodoma ambapo Wasomali 44 waligundulika kuwa wamekufa na 72 wakiwa wamenusurika.

Miili hiyo iliyokuwa imeanza kutoa harufu, 22 ilizikwa Dodoma na 22 ilizikwa Ijumaa wiki hii mjini Morogoro katika makaburi ya Kolla ilikopewa mazishi ya jumla ya Kikristo na Kiislam.
                     PICHA/HABARI:  DUNSTAN SHEKIDELE,  GPL, MOROGORO


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo