MELI YA KALAMA YAPIGWA STOP

Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi zanzibar

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imeipiga marufuku meli ya MV Kalama ambayo ni pacha na meli ya Skagit iliyozama baharini wiki iliyopita.

Uwamuzi huo umetangazwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, wakati akipokea misaada ya fedha kutoka Mfuko wa Pensheni wa watumishi wa Serikali za Mitaa na Radio Coconut.

Balozi Iddi amesema kuwa pamoja na kuisimamisha meli hiyo kutoa huduma za usafiri kwenye bahari ya Hindi, pia imewataka watu wote wanaotaka kununua meli kuleta kwanza aina na muundo wa meli wanayotaka kuinunua na imetumika kwa muda gani.

Lakini amesema meli ambazo zimeshaingia na kusajiliwa, nazo zinafanyiwa uchunguzi ili kubaini ubora na umri wake tangu ianze kufanya kazi kabla ya kuingizwa nchini kwa biashara ya kusafirisha abiria.

Hata hivyo amesema kuwa Serikali inajipanga kununua meli ya uhakika itakayotoa huduma ya usafiri majini kati ya Zanzibar na Pemba na Zanzibar na dar es Salaam ili kupunguza mashaka kwa wasafiri.

Mfuko wa Pensheni ya Watumishi wa Serikali za Mitaa NLPF kupitia Mkurugenzi wake Bw. Andrew Kuyeyama umetoa shilingi milioni 5 na Bw. Ali Khatibu Dai wa Radio Coconut ametoa mchango wa shilingi milioni moja zote zikiwa kwa ajili ya kusaidia gharama za matibabu na za mazishi kwa wafiwa.
0784 886488/ 0767 886488/ 0715 886488 INSP. MHINA


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo