Afisa
elimu ya sekondari katika halmashauri ya wilaya ya Singida Voster Mgina
akitoa taarifa ya kuungua kwa baadhi ya vitanda vya bweni la wasichana
wa shule ya sekondari ya Wembere kata ya Mugungira tarafa ya Sepuka.
Moja ya vitanda vya bweni la wasichana wa shule ya sekondari ya Wembere vilivyougua moto. (Picha zote na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu.
Bweni
la wanafunzi wa kike katika shule ya sekondari ya Wembere kata ya
Mugungira tarafa ya Sepuka jimbo la Singida Magharibi limenusurika
kuteketea kwa moto.
Mazingira
ya kutokea kwa moto huo ambayo ni ya kutatanisha, inadaiwa kwa wakati
huo wanafunzi 14 wa bweni hilo lenye uwezo wa kulaza wanafunzi 46
hawakuwepo ndani ya bweni hilo.
Akizungumza
na mwandishi wa habari wetu, Afisa elimu wa shule za sekondari
katika halmashauri ya wilaya ya Singida Voster Mgina, amesema moto huo
uliweza kuzimwa na wanafunzi wakishirikiana na walimu wao kwa kutumia
maji.
Amesema moto huo umeunguza vitanda viwili vya chuma aina ya ‘double decker’, magodoro mawili na nguo za mwanafunzi mmoja.
Mgina amesema kuwa chanzo cha moto huo bado hakijajulikana na upelelezi zaidi unaendelea ili kujua chanzo cha moto huo.
Wakati
huo huo, Mgina amesema hadi sasa shule hiyo yenye mabweni mawili yenye
uwezo wa kulaza wanafunzi 80, ni wanafunzi 22 tu wa kidato cha kwanza
waliokwisha kuanza masomo shuleni hapo.
Kwa hisani ya MO BLOG