KUWEKWA KAZINI KWA ASKOFU LEVIS SANGA NA MSAIDIZI WA ASKOFU KWAFANA MAKETE

 Askofu Levis Sanga akipewa uaskofu



 Askofu Levis (mwenye fimbo) akiwa na maaskofu wenzie

 Askofu Sanga akipongezwa na mkewe
 Mkuu wa Mkoa wa Njombe Kapt. Mstaafu Aseri Msangi akimpa mkono baba askofu
 Mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro akimpa mkono baba askofu


 Hapa msaidizi wa askofu akipewa usaidizi wa askofu


 Askofu Levis Sanga (kushoto) akiwa na Msaidizi wa Askofu Mch. Kahuka

 Mkuu wa KKKT Dkt Alex Malasusa (wa kwanza kushoto) akiwa na askofu Sanga na msaidizi wa askofu Kahuka pamoja na wake zao
 Askofu Sanga akitoa hotuba yake

RC NJOMBE

DC MAKETE





Askofu wa Dayosisi ya kusini Kati Mch. Levis Luhuvilo Sanga hii leo amesimikwa rasmi kuwa Askofu na mkuu wa Dayosisi hiyo pamoja na Mch. Philemon Kahuka kuwa msaidizi wa askofu wa dayosisi ya kusini kati

Tendo hilo limefanyika katika viwanja vya kanisa kuu Makete mjini na kuhudhuriwa na Mkuu wa kanisa la KKKT Dkt. Alex Malasusa, Mkuu wa mkoa wa Njombe ambaye pia alimwakilisha mgeni rasmi Mizengo Pinda, maaskofu mbalimbali na wasaidizi wao, mkuu wa wilaya ya Makete, viongozi mbalimbali wa dini pamoja na waumini wa madhehebu mbalimbali

Askofu aliyemaliza muda wake Dkt. Hans Mwakabana ndiye aliyeongoza tendo la kumsimika kazini Askofu Levis Sanga

Pia Mkuu wa Kanisa La kiinjili la kilutheri Tanzania Dkt. Alex Malasusa alimsimika askofu Levis Sanga kuwa mkuu wa Dayosisi ya kusini Kati

Baada ya tendo hilo Askofu Levis Sanga alimsimika kazini msaidizi wa askofu Mch. Philemon Kahuka

Kukamilika kwa tendo hilo la kuwasimika kazini viongozi hao zilifuata salamu mbalimbali ikiwemo hotuba ya askofu Levis Sanga pamoja na hotuba ya Mgeni rasmi waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa mkoa wa Njombe Kapten Mstaafu Aseri Msangi
Akitoa hotuba yake kwa mamia waliofurika katika viwanja vya kanisa kuu Makete mjini Askofu Sanga amesema kanisa litaendelea kushirikiana na serikali katika kutatua changamoto mbalimbali zikiwemo za afya na elimu kwani kwa sasa kanisa kupitia dayosisi ya kusini kati linaanzisha chuo cha ualimu Bulongwa kitakachotoa mafunzo ya ualimu kwa ngazi ya stashahada na cheti daraja la tatu A na chuo hicho muda wowote kuanzia sasa kitaanza kutoa mafunzo hayo

Pamoja na mambo mengine amesema kuwa kanisa linaendelea kutoa elimu ya namna wananchi watakavyotoa maoni yao katika mchakato wa kuanzisha katiba mpya kwani ni wajibu pia wa kanisa kufanya hivyo

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Njombe Kapten Mstaafu Aseri Msangi ambaye alimuwakilisha mgeni rasmi waziri mkuu Mizengo Pinda alianza kwa kumtambulisha mkuu mpya wa wilaya ya Makete Mh. Josephine Matiro pamoja na kuwahakikishia wananchi kuwa serikali inatambua mchango wa kanisa katika kusukuma gurudumu la maendeleo hapa nchini

Amesema kuwa  anakaribisha maoni ya wananchi kufanikisha maendeleo ya mkoa wa Njombe pamoja na kuhakikisha kuwa atasimamia urasimu uliopo katika kuanzisha taasisi mbalimbali hasa za kidini ikiwemo vyuo na shule ama hospitali

Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika kufanikisha sensa ya watu na makazi na kuwataka wananchi wote kushiriki ipasavyo

Akitoa shukrani kwa Mgeni rasmi Mkuu wa KKKT Dkt. Alex Malasusa amefurahishwa na ushirikiano uliooneshwa na Mkuu wa mkoa wa kushirikiana na kanisa na kuongeza kuwa lengo la kanisa ni kuhakikisha viongozi wote wanamjua Mungu ili wafanye kazi zao kwa uweza wa Mungu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo