MWANAMKE ALIYEMTUPA MTOTO CHOO CHA SHULE APATA DHAMANA.

MAHAKAMA ya wilaya ya Lindi,imempatia dhamana mshitakiwa Aluminata Alois Kimisa (38) anayekabiliwa na Shitaka la kujaribu kumuuwa mtoto wake mchanga aliyemzaa usiku wa mei 19 mwaka huu. 
 
Mwandishi kutoka Lindi Abdulaziz Video anaripoti kuwa ,Uamuzi wa kumpatia dhamana mshitakiwa huyo umetolewa mei 28 mwaka huu na Hakimu wa mahakama ya wilaya hiyo,Liliani Lugalabamo, baada ya kupitia vifungu mbalimbali vya Sheria.

Mshitakiwa Aluminata mei 22 mwaka huu,alifikishwa mahakamani hapo akikabiliwa na Shitaka la kujaribu kumuuwa mtoto wake kwa kumtumbukiza kwenye Shimo la Choo. 

Akitoa uwamuzi huo,Hakimu Lugabamo akitumia ibara ya 6 na 7 ya Human right alisema kila mtu ana haki sawa mbele ya Sheria,hivyo kutokana na mshitakiwa ana mtoto mchanga ambaye anatakiwa kuwa karibu zaidi na mama anampatia dhamana,huku akiamuru kupatiwa mtoto wake kwa ajili ya kumnyonyesha. 

Pia Hakimu huyo amemuagiza mshitakiwa huyo kuripoti mahakamani hapo kila siku ya ijumaa saa 2:30 asubuhi.
Mwanamke huyo amefikishwa katika mahakama ya mkoa huo,mei 22 mwaka huu,na kusomewa shitaka lake na mwanasheria wa Serikali, Juma Maige. 

Aluminata alitinga mahakamani hapo, akiwa amevalia nguo aina ya vitenge na kujifunika kanga huku kichwani akiwa amefunika nywele zake kwa mzura wa rangi ya kahawia,huku dada zake wakiwa wamekibeba kichanga hicho. 

Na www.francisgodwin.blogspot.com


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo