MAMA MBARONI KWA TUHUMA ZA KUMCHOMA MOTO MWANAYE


Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Doktafu Mbilinyi mkazi wa Ikonda wilayani Makete anashikiliwa na polisi wilayani Makete kwa tuhuma za kumchoma moto mtoto wake wa kumzaa

Kwa mujibu wa mkuu wa polisi wilaya ya Makete Bw, Peter Kaiza amesema tukio hilo lilitokea siku Juni 5 mwaka huu ambapo mama huyo alikamatwa katika hospitali ya Consolata Ikonda alikompeleka mtoto huyo kwa ajili ya matibabu  zaidi baada ya kuona ameshindwa kumtibu kwa njia za kienyeji

Kwa mujibu wa maelezo ya mama huyo amesema  mtoto wake aliungua moto wakati akicheza na mtoto mwenzie na si kama amemuunguza yeye

Mama huyo yupo nje kwa dhamana na muda wowote atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili

Na Veronica Mtauka, Teddy & Ester


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo