WANAMAKETE WAMSHAURI NAIBU WAZIRI MAHENGE


Siku kadhaa baada ya Naibu waziri wa Maji ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Makete Mh. Dkt Binilith Mahenge kutembelea wilaya ya Makete, wananchi wametoa ushauri wao kuhusiana na suala la barabara na umeme kama alivyozungumza na wananchi wa jimbo lake

Wakizungumza na Kitulo Fm baadhi ya wananchi hao wamesema wamefurahishwa na kauli hiyo ya Mh. Naibu waziri na kusema anatakiwa kuhakikisha inatekelezwa kwa wakati

Mkazi mmoja wa Makete aliyejitambulisha kwa jina la Andrea Sanga ambaye pia ni mfanyabiashara amesema amepokea vizuri kauli ya Mh. Naibu waziri na kuwataka wananchi kuwa na subira wakati huu wa kutekelezeka wa kauli aliyoitoa

Kwa upande wake Osia Mpandila amesema kauli hiyo ilimfurahisha na anaamini imewafurahisha wananchi wengi ikiwemo suala la upelekaji umeme katika eneo la Tandala ambao hatua zitaanza kuchukuliwa kuanzia mwezi Septemba mwaka huu

Mei 21 mwaka huu Naibu waziri wa Maji ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Makete alifanya ziara katika jimbo lake ambapo pamoja na mambo mengine alizungumzia suala la umeme na barabara katika jimbo lake


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo