Hayo
yamezungumzwa na mtendaji wa kijiji cha iwawa bw, Msigwa alipokuwa akizungumza
na MTANDAO HUU na kusema kuwa kuna baadhi ya watu wanachoma moto mashamba yao bila kibali na huwa
hawawi makini, kwani moto huo wakati mwingine unafika katika kuunguza uoto wa
asili na kupelekea uharibifu wamazingira
Amesema
wananchi wanatakiwa kuchukua kibali kutoka serikali ya kijiji kitakacho
wawezesha kuchoma mashamba yao
moto ili endapo kutatokea uzembe katika uchomaji huo na uharibifu wa mazingira
kutokea basi itakuwa rahisi kumpata na kumchukulia hatua za kisheria
Aidha
bw Msigwa amesema kwasasa inakuwa vigumu kuwakamata watu wanaotorosha moto kwa
kuwa watu hawachukui vibali hivyo ofisi
yake imepanga kudhibiti vitendo vya uchomaji moto kwa kuchukua hatua kali za kisheria