TUNAJALI MAKETE YAIKUNA SERIKALI

Shirika lisilo la kiserikali la Tunajali linalojihusisha na utoaji wa huduma kwa watu wanaoishi na vvu wilayani makete limepongezwa kwa kuhakikisha kila kijiji cha wilaya kina pata elimu ya kuhusu vvu na dawa za kupunguza makali ya virusi hivyo

Akitoa pongezi hizo mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya makete bw, Daniel Okoka amesema amefurahishwa na kazi zinazofanywa na shirika hilo la tunajali kwani wamefanikiwa kutoa elimu kwa vijiji vtote wilayani makete

Amesema wananchi wanatakiwa kuzitumia dawa hizo za kupunguza makali ya vvu kwani dawa ya kuuponya kabisa ugonjwa huo haija patikana na kuwaasa wasio na maambukizi kujikinga na kuwa waaminifu katika mahusiano yao

Aidha ameyaomba mashirika mengine kuiga mfano wa shirika la tunajali ili kuweza kupunguza maambukizi ya vvu wilayani makete na kuwataka pia wananchi kujihusisha na shughuli za kimaendeleo vijijini mwao kwani kwa kufanya hivyo kutawasaidia kuondokana na umasikini na kuweza kuinua kipato cha familia na wilaya

Na: Obeth Ngajilo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo