WAFUGAJI ACHENI UKAIDI

Wananchi wilayani Makete wameshauriwa kutopuuza maagizo yanayotolewa na madaktari wa mifugo kuhusu kupeleka mifugo yao kupatiwa chanjo na matibabu

Hayo yamezungumzwa na Daktari wa mifugo wilaya ya Makete Nuru Issae wakati akizungumza na wanahabari na kusema kuwa baadhi ya wananchi wamekuwa hawapeleki sehemu itolewapo chanjo au matibabu

Ameongeza kuwa kutopeleka mifugo kupatiwa matibabu ama chanjo kunapelekea wafugaji kutopata mazao mazuri yatokanayo na mifugo yao  ikiwemo maziwa, mbolea na nyama iliyo bora

Miongoni mwa magonjwa hayo ni ugonjwa wa ndiganakali ambao mara nyingi huwaathiri ngómbe, ambapo dalili za ugonjwa huo ni pamoja mnyama kupumua kwa shida na kupelekea kifo

Na Anitha Sanga


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo