TANZANIA BADO INASUASUA KUTIMIZA MALENGO YA MILENIA

DSM                   
Ikiwa imesalia miaka mitatu kabla ya mwaka 2015 ambapo nchi zinapaswa kufikia malengo ya milenia ikiwa ni pamoja na kupunguza vifo vya akina mama wakati wa kujifungua na vile vya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano tathmini ya madaktari bingwa wa masuala ya afya ya uzazi inaonesha kuwa kasi ya Tanzania katika kufikia malengo hayo si ya kuridhisha

Madaktari hao bingwa wa masuala ya uzazi wametoa tathmini hiyo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano wa mwaka wa madaktari bingwa wa uzazi na magonjwa ya wanawake AGOTA

Akifungua mkutano huo rais mstaafu wa awamu ya Pili Alhadji Ali Hassan Mwinyi pamoja na kuwapongeza madaktari hao kwa kazi nzuri amekiri kuwepo kwa changamoto katika kuboresha huduma za afya hapa nchini

Kauli mbiu ya mkutano huo ni vifo vya mama na magonjwa ya mtoto tunapofikia miaka 50 ya uhuru je tuko wapi?


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo