CHANJO YA WATOTO YAZINDULIWA MAKETE

Makete                                 
Wazazi na walezi wilayani Makete wametakiwa kuwapeleka watoto wao kwa wingi ili wapatiwe chanjo za magonjwa mbalimbali kwani kwa kutofanya hivyo ni kosa kisheria na hatua kali zitachukuliwa dhidi yao

Mkuu wa wilaya ya Makete Mh Zainab Kwikwega ameyasema hayo wakati akizindua wiki ya chanjo kiwilaya zoezi lililofanyika katika hospitali ya wilaya ya Makete

Mh. Kwikwega amesema kutowapeleka watoto kupatiwa chanjo ni kuwakosesha hakia yako ya kimsingi ya kukingwa na magonjwa mbalimbali

Kwa upande wake kaimu mganga mkuu wa wilaya ya Makete Carlo Makombe amesema kuwa zoezi hilo zoezi hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo umbali wa kuvifikia vituo vya afya

Akimshukuru mkuu wa wilaya Bi Ester Ngogo ambaye ni mratibu wa huduma za afya ya uzazi na mtoto amemshukuru Mkuu huyo wa wilaya kwa utayari wake wa kuzindua kampeni hiyo wilayani hapo

Kauli mbiu ya wiki ya chanjo ni “Mtoto asiyechanjwa ni hatari kwake mwenyewe na wengine mpeleke akapate chanjo”


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo