IKULU YAKANUSHA JK KUZUNGUMZA NA PINDA

Kurugenzi ya mawasilianao Ikulu jijini DSM imekanusha taarifa zilizochapishwa na gazeti moja la kila siku hapa nchini zinazodai kuwa kumekuwa na mazungumzo baina ya rais Jakaya Kikwete na Waziri mkuu Mizengo Pinda kuhusu hatua inayopaswa kuchukuliwa dhidi ya mawaziri wanaoshinikizwa kujiuzulu kwa madai kuwa utendaji kazi wao hauridhishi

Taarifa hiyo imesema rais Kikwete hajaonana wala kufanya mazungumzo yeyote na waziri mkuu Pinda kuhusiana na suala hilo  na kwamba hivi sasa Rais anasubiri kupata taarifa rasmi kutoka bungeni mjini Dodoma

Kwa mujibu wa taarifa hiyo habari iliyochapishwa katika gazeti hilo zinazodai kuwa rais Kikwete anawalinda baadhi ya mawaziri hao ambao wanataka kujiuzulu haina ukweli wowote na ni upotoshaji

Taarifa hiyo imewataka wananchi kutoamini habari hiyo na kutaka wanahabari kuzingatia weledi wanapofanya kazi zao

Wakati huo huo rais Jakaya Kikwete yupo mjini Blantaya Malawi kwa ajili ya kuhudhuria maziko ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo Marehemu Prof. Bingu wa Mutharika aliyefariki April 5 Mwaka huu kwa baada ya kuugua ugonjwa wa moyo

Rais Kikwete ni miongoni mwa viongozi wakuu 7 kutoka nchi jirani na Malawi walioshiriki maziko hayo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo