KONGAMANO LA PASAKA KWA WANAFUNZI MAARUFU KAMA EASTER CONFERENCE LAFUNGULIWA WILAYANI MAKETE

MAKETE                 

Jumuia  ya wanafunzi  kutoka  katika  makanisa  ya  kipentekoste Tanzania CASFETA wilayani  Makete  wamefungua  rasmi  kongamano  la  Pasaka  (EASTER CONFERENCE katika  Ukumbi  wa  Shule  ya  Sekondari  ya  Iwawa.

Akifungua  kongamano  hilo Mwangalizi  wa  Makanisa  ya  Tanzania  Assembles  of God sehemu  ya Tandala Mch. JONASI SANGA amekemea  vitendo viovu vinavyofanywa miongini  mwa wanafunzi  kitendo  alicho  kiita  ni dhami.

Amevitaja  vitendo  viovu  vinavyofanywa  na  wanafunzi  mashuleni  kuwa  ni pamoja  na ulevi  uashereti, wizi pamoja  na vurugu wanapokuwa  mashuleni na kuwasihi kuwa waadilifu kwa  walimu  na wazazi pamoja  na kuwa na juhudi katika  masomo yao

Katika hatua nyingine ametaka wanafunzi  waliookoka kuwa mfano wa kiugwa na kutumia  maandiko matakatifu  kama  silaha  yao ya imani  ya  kikristo na kuongeza kuwa Biblia imeandikwa  shika sana  Elimu  usimwache  aende zake, hivyo wanafunzi hao wazingatie elimu
Na Aldo Sanga & Anitha Sanga


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo