KIKAO CHA MCHAKATO WA NJOMBE PRESS CLUB CHAFANYIKA MKOANI NJOMBE




 Hapa kikao kikiendelea Dosmeza Hotel
Aldo Sanga(kushoto) wa Kitulo Fm akiwa na Shaaban Lupimo wa Uplands FM

Neema Mwanga (kushoto) kutoka Best Fm Ludewa akiwa na Magreth Lupembe

 Aldo Sanga akiandika kumbukumbu za kikao hicho
Huyu amaa alinivutia kupiga naye picha

Baada ya kikao


Friday Simbaya kutoka Nipashe naye alikuwepo

Edwin Moshi kutoka Kitulo Fm


Waandishi wa habari mkoa mpya wa Njombe wamelalamikia kitendo cha taarifa za upotoshaji mchakato wa kuanzisha chama cha waandishi wa habari mkoa wa Njombe (Njombe Press Club) zilizotolewa na moja ya mwandishi maarufu mkoani humo ambaye jina linahifadhiwa kuwa kikao kilichokuwa kimepangwa kufanywa na wanahabari hao hakipo

Wakizungumza na mtandao huu baadhi ya waandishi hao wamesema mahudhurio finyu ya waliohudhria kikao hicho yamesababishwa na taarifa zilizotolewa na mwandishi huyo kwakuwapigia simu waandishi wengi kuwa kikao hicho kimeahirishwa kumbe si kweli

Kikao hicho ambacho kilifanyika kwenye ukumbi wa Dosmeza hotel kilijadili mambo mbalimbali kuhusu mchakato wa kuanzisha Njombe Press Club

Kikao kijacho kimepangwa kufanyika Jumamosi 14.04.2012 kuanzia saa nne asubuhi katika ukumbi wa Dosmeza Hoteli Mkoani Njombe ambapo viongozi mbalimbali wa Iringa Pres Club wanatarajiwa kuhudhuria kikao hicho

Waandishi kutoka Uplands Fm, Best Fm, Kitulo FM, Nipashe na wengine kutoka Njombe walihudhuria kikao hicho


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo