KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI KOROGOGWE YAZURU WILAYA YA MAKETE

MAKETE                 
Wajumbe wa kamati ya kudhibiti Ukimwi wilaya ya Korogwe mkoani Tanga wamefanya ziara ya siku mbili wilayani Makete kwa lengo la kujifunza mbinu mbalimbali za kuzuia maambukizi mapya ya vvu na Ukimwi  zinazofanywa na wilaya ya Makete

Katika ziara hiyo iliyojumuisha viongozi mbalimbali kutoka wilaya ya Korogwe akiwemo Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo Mh. Kallaghe Yusuph, pia ameambatana na baadhi ya madiwani, wawakilishi wa watu waishio na VVU, Maafisa wa Serikali pamoja na Viongozi wa Dini.

Mh. Kallaghe ametoa pongezi  kwa wadau  pamoja  na Serikali  ya Makete kwa hatua ambayo wamefikia  katika mapambano ya Ugonjwa wa ukimwi ambao kwa sasa unaendelea kupungua kwa kasi kubwa wilayani Makete ukilinganisha na miaka michache iliyopita ambapo Makete ilikuwa katika kiwango cha juu cha maambukizi ya vvu ukilinganisha  na wilaya zingine hapa nchini.

Katika  hatua  nyingine wanakamati hao wametembelea  baadhi ya  vijiji vikiwemo Ivalalila kilichopo katika kata ya  Iwawa pamoja na Kijiji cha Iniho kilichopo katani Iniho ambako waliweza  kufanya  mazungumzo  na wananchi wa vijiji hivyo ili kujifunza zaidi namna wanavyojikinga na maambukizi mapya ya vvu, ambapo walijifunza namna waviu wanavyotoa elimu kwa watu mbalimbali kupitia vikundi vyao

Wajumbe hao waametoa shukrani kwa ushirikiano walioupata kutoka kwa viongozi wa Halmashauri kwa Kufanikisha  zoezi la  kujufunza na kubadilishana uzoefu na namna walivyoweza kupambana na maambukizi mapya  ya  VVU na Ukimwi  Wilayani  Makete.
Na Aldo Sanga.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo