DIWANI ALIA NA UKOSEFU WA MTAALAMU WA AFYA KATANI MWAKE

MAKETE                                        
Wakazi wa kata ya Kiguru tarafa ya Magoma wilayani Makete wamemuomba mganga mkuu wa wilaya ya Makete kuwapelekea muuguzi wa afya aliyepangiwa kufanya kazi kijijini hapo kwa ajili ya kutoa huduma za kiafya

Akizungumza na Mwandishi wa habari hii Diwani wa kaya ya Kiguru Mh. Simion Mwaikenda ameshangazwa na hatua ya kutopelekewa muuguzi huyo wa afya mpaka sasa kwani kijiji hicho kipo tayari kumuandalia makazi mazuri

Nao wananchi wa kata hiyo wamelalamikia adha wanayoipata kwa kukosa huduma ya afya kijijini kwao
Naye kaimu mganga mkuu wa wilaya ya Makete Dkt Ahmad Shaaban amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kuahidi kwenda kukagua nyumba atakayoishi mhudumu huyo ambayo imeandaliwa na wanakijiji hao, na endapo itakidhi viwango stahili atampeleka muuguzi huyo pamoja na madawa

Na Veronica Mtauka


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo