Watu 60 wamekufa mkoani Lindi

LINDI
Watu 60 wamekufa mkoani Lindi katika ajali 193 za barabarani zilizotokea kati ya Januari na Desemba mwaka jana huku wengine 310 wakijeruhiwa ambapo baadhi yao wamepata ulemavu wa kudumu

Hayo yamebainishwa na kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Lindi George Mwakajinga ambapo amebainisha kuwa idadi hiyo ya vifo imepungua ikilinganishwa na vifo 72 vilivyotokea mwaka 2010 katika ajali 172 zilizosababisha majeruhi 275

Amesema kati ya ajali hizo 48 wahusika wamefikishwa mahakamani ambapo wamepatikana na hatia na kupewa adhabu mbalimbali 35 bado zipo mahakamani 28 zimefutwa na zilizosalia 82 bado uchunguzi unaendelea


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo