Wanawake wilayani Makete wametakiwa kuuwatunza watoto yatima na kuwapa mahitaji muhim bila ubaguzi

Hayo yamezungumzwa na mwanawake anaye jishughulisha na biashara ndogondogo wilayani hapo ambaye hakutaka jina lake litajwe na kusema kuwatunza watoto yatima nakuwapa mahitaji muhimu itasaidia kuepukana na watoto  wa mitaani  na kuwafanya watoto hao kuishi kwa amani

Hata hivyo amesema baadhi ya wanawake wamekuwa hawawathamini watoto yatima nakupelekea baadhi ya watoto hao kuamua kuishi maisha ya kujitegemea hali inayo pelekea kuona maisha magumu na kujiingiza katika makundi mabaya kama wizi, na ulevi.

Aidha amewataka wananchi waone umuhimu wa  kuwapeleka watoto yatima shule ili kuwajenga kielimu

NA ZUHURA SANGA


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo