Wakazi wa kijiji cha Kitivo kata ya Kerenge Korogwe vijijini, wamondokana na tatizo la maji

Wakazi wa kijiji cha Kitivo kata ya Kerenge Korogwe vijijini, wameondokana na tatizo la uhaba wa maji katika eneo hilo kufuatia kuzinduliwa kwa mradi wa maji ambao utahudumia wakazi zaidi ya 1,600 ikiwa ni sehemu ya mafanikio ya maadhimisho ya wiki ya maji nchini

Akizungumzia uzinduzi wa mradi huo mkuu wa wilaya hiyo Erasto Sima, amewataka wanakijiji hao kutunza miundombinu ya maji ili mradi huo uwe endelevu kwa manufaa ya wakazi wa eneo hilo

Vituo saba vya kuchotea maji kila kimoja kina uwezo wa kuhudumia watu 250

Uzinduzi huo umekwenda sambamba na maadhimisho ya wiki ya maji kama anavyozungumza mkuu wa wilaya hiyo

Nao baadhi ya wananchi wa korogwe  waliokuwa wakipata shida ya kukosa maji walishukuru kwa uzinduzi huo kwani unafuu wataupata

WAKATI HUO HUO

Jijini Tanga nako wamezindua maadhimisho ya wiki ya maji

Kaimu mkurugenzi wa mamlaka ya maji safi na maji taka Jamal Ngereja katika wiki hii ya maadhimisho ya wiki ya maji wametoa ofa kwa wateja wao

Amesema wateja waliokatiwa maji muda mrefu pia watatembelewa ili kuangalia namna ya kuweza kuwarejeshea huduma ya maji kwa kufuata taratibu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo