KIBAKA AIBA SIMU DUKANI, JIONI AMPORA SIMU MCHEZAJI WA SIMBA MORO



WANANCHI katika Manispaa ya  Morogoro wamelitupia lawama jeshi la polisi mkoani hapa kwa kitendo chao cha kumuachia kijana aliyeonekana kuwa  kibaka mzoefu wa simu ambaye baadaye walimwachia baada ya kukamatwa kuiba simu majira ya mchana katika dula la mfanyabiashara mjini Morogoro.

 Kijana huyo ambaye alipewa mkong'oto mkali na wananchi aliokolewa na polisi ambaye waliondoka naye pamoja na mmilikiwa duka hilo la simu.

 Katika hali ya kushangaza, kijana huyohuyo jioni alimpora simu Mwinyi Kazimoto, mchezaji wa timu ya Simba iliyokuwa ikicheza na timu ya Mtibwa Sugar ya Morogoro katika mchezo wa Ligi Kuu.

 Kibaka huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana alipora simu hiyo baada ya mechi hiyo.

 Hata hivyo mchezaji wa Simba, Uhuru Selemani, alisaidiana na kiongozi wa klabu hiyo,
Geoffrey Nyange, kumfukuza kibaka huyo na kufanikiwa kumkamata na kumwangushia kichapo kwa kusaidiana na mashabiki wa soka waliokuwa uwanjani.

 Kibaka huyo aliokolewa tena na polisi ambao waliondoka naye.
source:Global publishers


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo