NMB MAKETE YALALAMIKIWA

Wananchi wilayani Makete ambao ni wateja wa NMB wamelalamikia usumbufu unaowakumba  katika kupata huduma za benki ya NMB tawi la Makete  wakati mtandao haupo.

Wateja hao wakizungumza na mtandao huu wamesema kukosa huduma za kuweka na kutoa fedha ilipelekea usumbufu kwao pamoja na kukwamisha shughuli zao za kimaendeleo.

Akizungumzia tatizo hilo, mmoja wa wafanyakazi wa benki hiyo ya NMB tawi la Makete ambaye hakutaka jina lake litajwe redioni amesema hali hiyo inatokana na kukatika kwa mtandao wa Vodacom ambao wanashirikiana katika kutoa huduma za kibenki kwa wateja

Hata hivyo amebainisha huduma hizo zinaendelea kutolewa japo sio kwa ufanisi wa uhakika.

Zuhura&Godson


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo