MALALAMIKO YA WAFANYABIASHARA

Mji wa Makete

MAKETE                               22.02.2012

Wafanyabiashara wa soko la wakulima Makete  Mjini wametoa kero kubwa wanayoipata pindi wanapohamishwa kila mwisho wa mwezi kwenda kwenye mnada katika soko la Ngiu wilayani hapa

Wakizungumza na Kitulo Fm sokoni hapo wafanyabiashara hao ambao hawakupenda majina yao yatajwe wamesema wakienda kuuza bidhaa zao katika mnada huo, bidhaa hizo hazinunuliwi kama wanavyotaka hali inayowasababishia kupata hasara

Kutokana na hali hiyo wameiomba serikali kutafuta wafanyabiashara wakubwa ili wanunue bidhaa zao kwa jumla kuliko ilivyo sasa ambapo bidhaa zao huuzwa kwa reja reja

Kwa upande wake Afisa biashara na masokao wilaya ya Makete Bw. Edonia Mahenge ameahidi kuwahamasisha wafanyabiashara kutoka Njombe na Makambako kuja kununua bidhaa za wafanyabiashara wa Makete kwa bei za jumla na rejareja

Hata hivyo amewataka wafanyabiashara hao kuendelea kupeleka bidhaa zao katika mnada huo, kwani wafanyabiashara mbalimbali kutoka nje ya wilaya ya Makete hununua bidhaa nyingi hali inayowasaidia kutopata hasara


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo