UTALII WA NDANI MAKETE BADO HALI TETE


MAKETE          22.02.2012

Wananchi wilayani Makete wameshauriwa kujiwekea mazoea ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Kitulo pamoja na vivutio mbalimbali vya kitalii ikiwemo pori la akiba la mpanga kipengele

Hayo yamezungumzwa na Afisa maliasili wilaya ya Makete Bw. Uhuru Mwembe alipokuwa akizungumza na Kitulo Fm na kuongeza kuwa mwitikio wa wanamakete kutembelea vivutio hivyo bado hauridhishi ukilinganisha na watalii wa nje

Amesema wilaya ya Makete imebahatika kuwa na hifadhi ya Kitulo ambayo ina vivutio kama uwanda wa nyasi, milima pamoja na maporomoko ya maji lakini bado wanamakete hawana utaratibu wa kutembelea maeneo hayo

Aidha Bw. Mwembe amewataka wananchi wa Makete kuanza kujiwekea utaratibu wa kutembelea hifadhi hiyo kwani kwa kufanya hivyo watajifunza mambo mbalimbali ambayo hawayafahamu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo