KIDUMU KUJENGA UKUMBI KWAO BURUNDI


Mwanamuziki  Jean Pierre Nimbona ‘Kidum’ amesema kuwa anafikiria kujenga uwanja mkubwa wa burudani utakaokuwa na shughuli nyingi nchini Burundi Kidum, aliyasema hayo baada ya kuvutiwa na muundo wa uwanja wa kisasa wa burudani wa Dar Live, uliopo Mbagala Zakhem, Dar es Salaam.
Dar Live ni uwanja wenye vivutio vingi, kama vile michezo ya watoto, jukwaa kubwa la kisasa lenye mfumo bora kabisa wa sauti, taa za kiwango cha juu, huku pia kukiwa na eneo kubwa la burudani, vitu ambavyo vimemgusa Kidum.“Huu ni uwanja mkubwa sana.
Unavutia na kwa kweli ukiwa hapa mwanamuziki anafurahia kutoa shoo,” alisema Kidum.Aliongeza: “Nitajenga Burundi lakini tatizo kule ni amani. Unaweza kuandaa kitu kizuri lakini matokeo yake watu wakavamia na risasi.”...
NA PRO 24DJS


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo