BEI YA KUKOBOA NA KUSAGA NAFAKA WILAYANI MAKETE YAPAA MARA DUFU

Mkuu wa wilaya ya Makete Mh Zainab Kwikwega amewataka wfanyabiashara wa kusaga na kukoboa nafaka wilayani Makete kushusha bei za kukoboa na kusaga nafaka kutokana na wao kupandisha zaidi ya asilimia mia moja

mkuu huyo wa wilaya ametoa kauli hiyo wakati akifungua kikao cha baina ya uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Makete na wafanyabiashara hao kukao kilichofanyika kwenye ukumbi wa HIMA Makete

Mkuu hyuo ameongeza kuwa ni wakati wa wafanyabiashara hao kutumia busara katika kupata suluhu ya bei kwani imepanda kutoka sh.700 kwa kukoboa/kusaga debe moja ya nafaka hadi sh.1,500

ameongeza kuwa imekuwa kawaida kwa wafanyabiashara wilayani Makete kuuza mara dufu ya bei ya kawaida ya bidhaa au mara tatu

Kwa upande wao wafanyabiashara hao wamesema kupanda kwa gharama za umeme na maji ni moja ya sababu kubwa inayopelekea wao kupandisha gharama ya kusaga na kukoboa nafaka

Kikao hicho kilichohusisha viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa wilaya ya Makete, Mkurugenzi mtendaji halmashauri wa wilaya ya Makete Imelda Ishuza, Afisa biashara wa wilaya pamoja na wadau mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara hao, hadi nakwenda mitamboni wamekubaliana bei elekezi iwe kati  ya sh. 1000 hadi 1200, na bei hiyo itapelekwa ofisini kwa mkuu wa wilaya kwa maamuzi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo