MAUAJI MAKETE

Makete                                     21.01.2011

Bw. Kawaida Ngigwa (75) mkazi wa kijiji cha Uganga kata ya Bulongwa wilayani Makete amekutwa akiwa amechinjwa  nyumbani kwake

Akizungumza na Kitulo Fm ofisini kwake Mkuu wa jeshi la Polisi wilaya ya Makete Bw. Rashidi Lundilo amesema tukio hilo limetokea tarehe 19/01/2011 majira ya asubuhi nyumbani kwa marehemu

Bw. Lundilo amesema kuwa akiwa nyumbani kwake marehemu Kawaida amekutwa ameuwawa kwa kukatwa shingo na silaha yenye ncha kali na watu wasiojulikana

Amesema kuwa baada ya polisi kuuchukua mwili wa marehemu  na kwenda kuuchunguza walibaini kuwa mwili wa Bw. Kawaida ulikuwa umetolewa ulimi na kuongeza kuwa kifo chake kinahusishwa na imani za kishirikina

Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo na linawaomba wakazi wa Uganga kuwa anayefahamu aliye husika na tukio hilo kutoa taarifa kwa jeshi hilo na wao watamlinda kwa kutomtaja.


By Edwin Moshi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo