Wapofuka macho baada ya kunywa pombe


Wanaume wawili wanaripotiwa kupoteza uwezo wa kuona baada ya kunywa pombe haramu katika kaunti ya Kirinyaga huku vita dhidi ya mihadarati vikichacha Mlima Kenya.


Kwa mujibu wa kamishna wa kaunti ya Kirinyaga Naiyoma Tobiko, wawili hao ni Julius Munene mwenye umri wa miaka 28 na Joseph Bundi mwenye umri wa miaka 45.


Kamisha Tobiko amewasihi wakaazi kutotumia pombe haramu akisema kuwa ni hatari kwa afya yao na kutoa onyo kali kwa wote wanaoendeleza biashara hiyo.


"Nani amekwambia pombe unayokunywa na dawa za kulevya unazotumia ni nzuri kwa afya ya bindamu? Pamoja na serikali ya kaunti, vita dhidi ya pombe hizo vitaendelea hadi pale ambapo zitafukuwa kabisa kutoka Kirinyaga," Tobiko alimaka. 

Chanzo:tukokiswahili



JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo