Wanaume wawili wanaripotiwa kupoteza uwezo wa kuona baada ya kunywa pombe haramu katika kaunti ya Kirinyaga huku vita dhidi ya mihadarati vikichacha Mlima Kenya.
Kwa mujibu wa kamishna wa kaunti ya Kirinyaga Naiyoma Tobiko, wawili hao ni Julius Munene mwenye umri wa miaka 28 na Joseph Bundi mwenye umri wa miaka 45.
Kamisha Tobiko amewasihi wakaazi kutotumia pombe haramu akisema kuwa ni hatari kwa afya yao na kutoa onyo kali kwa wote wanaoendeleza biashara hiyo.
"Nani amekwambia pombe unayokunywa na dawa za kulevya unazotumia ni nzuri kwa afya ya bindamu? Pamoja na serikali ya kaunti, vita dhidi ya pombe hizo vitaendelea hadi pale ambapo zitafukuwa kabisa kutoka Kirinyaga," Tobiko alimaka.
Chanzo:tukokiswahili
