IGP Sirro akabidhiwa gari mpya

Jeshi la Polisi Tanzania limemuaga rasmi aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Mstaafu Balozi Simon Nyakoro Sirro, leo tarehe 10 Mei 2023 baada ya kustaafu Utumishi ndani ya Jeshi la Polisi kwa mujibu wa sheria mwezi Machi 2023 ambapo baada ya kuagwa amekabidhiwa gari mpya (Zero KM) ambayo ataitumia katika maisha yake yote kipindi akiwa nje ya Utumishi wa Jeshi la Polisi.


Sherehe za kumuaga IGP Mstaafu Balozi Simon Nyakoro Sirro zimefanyika katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Dares Salaam (DPA) kilichopo Kurasini Jijini Dar es salaam kwa gwaride maalum la kumuaga ikiwa ni utaratibu wa Jeshi la Polisi kuwaaga kwa gwaride maalum Viongozi wa Polisi waliofikia cheo cha Kamishna wa Polisi na Inspekta Jenerali wa Polisi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo