Polisi wamsaka mchungaji aliyeshawishi waumini wafunge ili waende mbinguni kumuona YESU

Jeshi la Polisi katika Kaunti ya Malindi nchini Kenya linamtafuta Mchungaji Paul Mackenzie wa Kanisa la Good News International kutokana na kudaiwa kuwashawishi waumini wake wafunge kisha wafe ili waweze kuingia mbinguni na kuurithi ufalme.


Taarifa za awali zinaeleza waumini wanne wamefariki wakati wakipatiwa matibabu katika Hospitali Kuu Kaunti Ndogo ya Malindi, huku mmoja amefariki baada ya kufikishwa katika kituo cha Polisi cha Lango Baya ambako walipelekwa kwa ajili ya kutoa maelezo.

Polisi wamefanya msako baada ya kupokea taarifa kutoka kwa wasamaria wema kuhusu kuwepo kwa kanisa hilo lenye kueneza imani potofu kwa kuelekeza watu kufunga kisha wafe ili waweze kufika mbinguni.

Wakazi wa eneo la Shakahola, Kata ya Adu wamesema kwamba mhubiri huyo amekuwa akiwashawishi waumini wake wafunge bila kula, wafe ili waweze kuurithi ufalme wa mbinguni.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo