Majaliwa azindua mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2023





Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amezindua mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa kwa mwaka 2023, zilizofanyika katika uwanja wa Chama Cha Mapinduzi – CCM, wa Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara.

Mbio hizo, zimezinduliwa hii leo Aprili Mosi, 2023 ambapo viongozi kadhaa walihudhuria zoezi hilo akiwemo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Prof. Joyce Ndalichako.

Wengine ni Katibu Mkuu Ofisi wa Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Prof. Jamali Katundu na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed Abbas Ahmed na Wananchi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo