Mchungaji Kimaro arejea tena KKKT Kijitonyama


Shangwe na nderemo vimetawala katika Kanisa la KKKT Usharika wa Kijitonyama wakati wa ibada ya asubuhi (morning Glory) baada ya mchungaji, Dk Eliona Kimaro ambaye kurudi kutoka likizo aliyopewa.



Usiku wa Januari 16, 2023 ilisambaa video ikimuonyesha mchungaji Kimaro akiwaeleza waumini wake kuwa amepewa likizo ya siku 60 baada ya kuitwa katika ofisi ya msaidizi wa askofu na kufanya kikao na mkuu wa jimbo.

Dk Kimaro ambaye ni mchungaji kiongozi wa Usharika huo ameripoti usharikani hapo leo Ijumaa Machi 17, 2023 baada ya kumalizika kwa likizo ya siku 60 na kuibua furaha alipowasalimia waumini na kuwashukuru.

Hata hivyo Februari 19 Askofu wa KKKT, Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dk Alex Malasusa alitangaza kumsamehe mchungaji Kimaro.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa ibada hiyo Dk Kimaro amewashukuru waumini wa usharika huo kwa uvumilivu kwa kipindi chote alichokuwa kwenye nyumba ya malezi huku akitangaza ratiba za ibada ya Kwaresma kwa siku zilizobaki.

Waumini walioshiriki ibada hiyo wameshindwa kujizuia kwa furaha walizokuwa nazo kila alipokuwa akizungumza walinyanyuka na kushangilia na wengine kurusha maua.

Tazama video hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo