Mke wa Mwenyekiti abakwa na kuuawa Kagera


Mke wa mwenyekiti wa mtaa wa National Housing kata Rwamishenye katika manispaa ya Bukoba mkoani Kagera, Khadija Ismail (29) amebakwa na kisha kuuawa kwa kupigwa kwa kitu butu kichwani na kijana aliyetambulika kwa  jina la Paschal Kagwa (22) aliyekuwa akiishi naye.


Tukio hilo la kinyama limeripotiwa kutokea jana Jumatatu, Februari 13, 2023 majira ya jioni.

Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Erasto Sima amesema kuwa kijana anayetuhumiwa kumbaka mama huyo alikuwa akiishi nyumbani kwa mwenyekiti baada ya kupewa hifadhi. "Aliishi nao nyumba moja lakini sio ndugu yao alipewa hifadhi tu." 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo