Mahakama ya Wilaya ya Musoma mkoani Mara, imewahukumu mama na mtoto kifungo cha mwaka mmoja jela kila mmoja kwa kosa la kumzuia Afisa wa Sensa, Evody Rwechungura kutekeleza majukumu yake ya Sensa.
Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Hadija Masala anasema watu hao wametenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 43 kifungu kidogo cha 3 a na b2 cha Sharia ya Takwimu Sura ya 351 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2019.