Bibi Harusi Avaa Shela jeusi kwenye harusi yake

 

Bibi harusi kutoka Nigeria kwa sasa anavuma kwenye mitandao ya kijamii baada ya picha zake za harusi kusambaa mtandaoni.

Katika picha hizo, bibi harusi huyo aliyetambulika kwa jina la Dasplang Rinset Lisa, ameamua kubadilisha tamaduni ya kuvalia gauni jeupe kwenye harusi na kuvaa gauni jeusi na alionekana kupendeza ndani yake.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Lisa alifichua kwamba watu wengi walimuuliza maswali mengi kuhusu kwa nini aliamua kuvaa nguo nyeusi siku ya harusi yake.

“Nilipata maswali mengi kuhusu kwa nini nilichagua kuvaa gauni jeusi kwenye harusi yangu. Sawa nina majibu mengi ya maswali, hili nitaandika baadaye, lakini kwa sasa kuna mtu yeyote anaweza kuniambia kwa nini atapendelea gauni jeupe na kwa nini asipende rangi nyingine yoyote ya mavazi?” alimaka.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo