Waandishi wa habari wazuiwa uchaguzi CCM Kagera

Baadhi ya waandishi wa habari wamezuiliwa kuingia kwenye ukumbi wa uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Kagera huku ikielezwa kuna waandishi wamealikwa kwa ajili ya kuandika habari katika uchaguzi huo.


Mmoja wa watu waliokuwa mlangoni akiruhusu wajumbe kuingia ukumbini katika uchaguzi huo unaofanyika leo Jumanne, Novemba 22, 2022 amekuja na majina ya vyombo vitano akisema waandishi wake wanaruhusiwa kuingia ukumbini huku wengine wakizuiliwakuingia.

Katibu wa CCM mkoa wa Kagera, Christopher Palangyo alipofuatwa na waandishi hao alidai wasubiri watapata utaratibu badaye na hadi wagombea wanajinadi waandishi hao walikuwa nje ya ukumbi.

Wagombea nafasi ya uenyekiti CCM Mkoa wa Kagera ni Novatus Nkwama, Medard Mshobozi, Nazir Kalamagi na Kostansia Buhiye na msimamizi wa uchaguzi huo ni Spika wa Bunge la Tanzania, Dk Tulia Akson.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo