Mtoto wa mwaka mmoja auawa na mbwa

Mtoto wa mwaka mmoja ameumwa na mbwa aina ya pit bull hadi kufa katika jimbo la Eastern Cape nchini Afrika Kusini, kulingana na ripoti za vyombo vya habari nchini humo.


Mazingira ya shambulio hilo bado hayajabainika lakini mbwa huyo anaaminika kuwa wa jirani, shirika la utangazaji la SABC linaripoti.


Mtoto huyo alikimbizwa katika kituo cha afya lakini alifariki wakati matabibu walipokuwa wakimhudumia, mtangazaji huyo alisema.


Hili ni shambulio la tatu chini ya kipindi cha wiki moja, tovuti ya habari ya IOL inaripoti.


Kumekuwa na hasira ya umma kuhusu ripoti za mbwa kushambulia na kuua watoto katika wiki za hivi karibuni.



JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo