Shirika la umeme Tanzania
(TANESCO) wilaya ya Makete mkoani Njombe limeelezea kusikitishwa na
vitendo vya moto unaoanzishwa na baadhi ya watu ambao umekuwa ukiunguza
miundombinu yake na kusababisha hasara kwa shirika hilo
Akizungumzia suala hilo kwenye kikao cha baraza la
Madiwani wa halmashauri hiyo, Meneja wa TANESCO wilaya ya Makete Henricko Renatus
amesema kumekuwa na uharibufu unaosababishwa na watu kuchoma moto na kuunguza
nyaya na nguzo hali inayopelekea umeme kukatika na wao kubeba lawama
Amesema hali hiyo inasababisha fedha zinazotolewa
kwa ajili ya maboresho mbalimbali ya umeme, kuacha kufanya kazi iliyokusudiwa
na matokeo yake fedha hizo zinapelekwa kutengeneza miundombinu iliyoharibiwa na
moto na kusababisha mambo mengine kukwama, hivyo kuwaomba madiwani kuwasaidia
kuwaelimisha wananchi
Gwerino Mwasanga ni
Diwani wa kata ya Ikuwo na Christopher Fungo ni diwani wa kata ya Iniho
wamezungumzia suala hilo la moto lilivyoleta athari ikiwemo kuunguza
miundombinu ya Tanesco na hata uharibifu wa mazingira, huku pia wakitoa ushauri
kwa shirika hilo wanapofanya usafi wa njia ya umeme kwa kukata miti, yale
masalia wayaweke mbali na miundombinu hiyo ili moto ukija na kukuta hakuna
matawi ya miti madhara huwenda yakapungua

Hivi karibuni
kumeripotiwa matukio ya moto kuunguza miundombinu ya umeme katika maeneo
mbalimbali lakini pia na kuunguza misitu ya watu jambo linalochangia athari
kubwa na kwa upande wa Wilaya hatua mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa ikiwemo
uzinduzi wa kamati za kupambana na matukio ya moto zilizozinduliwa hivi
karibuni na mkuu wa Wilaya ya Makete.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi