Kilichowafanya wakutane na dhahama hiyo ni kutokana na kutuhumiwa kuiba vitu mbalimbali kwenye maduka na nyumba za watu katika mtaa huo
Kwa mujibu wa Mashuhuda wa tukio hilo akiwemo Dorisi Mchami, na Blandina Kayombo wameeleza kuwa mtoto wa mama huyo amekuwa akiiba vitu mbalimbali zikiwemo laptop, flash na vifaa vya simu pamoja na nguo zilizoanikwa majumbani na kumpelekea mama yake ambaye amekuwa akitafuta wateja na kuuza ili kupata fedha za kujikimu huku vitu vingine wakivitumia nyumbani kwake
Wamesema mara baada ya kumkamata mtoto huyo aliweza kuwapeleka nyumbani kwao anakohifadhi lakini hawakuvikuta mpaka walipotoa adhabu kwa mama yake na kuamua kuonesha alikokuwa amevifukia shambani nje ya nyumba yake kutokana na kuhofia kukamatwa
France Sanga ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Kambarage amesema katika mtaa wake suala la ulinzi ni la mtu mmoja mmoja kwa kuwa askari walionao hawatoshi na kudai katika mtaa wake wezi na wadokozi wapo.



