Majambazi wasimamisha mahubiri kanisani na kuwaibia waumini

Majambazi waliokuwa na silaha wamevamia kanisa huko Johannesburg nchini Afrika Kusini na kuwapora waumini huku wakiwatisha kwa bunduki, Jumamosi Novemba 26 mwaka huu.


Kamera ya kanisa hilo iliwanasa majambazi hao ambao walisimamisha ibada na kuanza kukusanya pesa na vitu vya thamani kutoka kwa watu waliohudhuria ibada katika kanisa la SDA la Johannesburg Central,


Viongozi wa kanisa hilo baadaye walituma ujumbe wa kuwafariji waumini wao na kuwataka kuhudhuria ibada ya ushauri siku ya Jumapili, siku moja baada ya tukio hilo.


”Kanisa linapenda kuchukua nafasi hii kuwahakikishia kuwa hili nalo litapita. Hakuna kinachodumu milele. Kama viongozi, tunaombea kanisa kuungana katika nyakati kama hizi tukisaidiana kimaadili na kimatendo,” umesema ujumbe huo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo