Kilichowapata waliotaka kumuua mama yao kwa nyundo

Mahakama ya hakimu mkazi Njombe imewahukumu kutumikia kifungo cha miaka 10 gerezani Focus lutengano na Aizack Lutengano baada ya kuwakuta na hatia ya kujaribu kumua mama yao mdogo Rehema Ngimbudzi mkazi wa kijiji cha mtwango wilayani Njombe kwa kumpiga na nyundo kichwani.


Akisoma hukumu hiyo katika kikao cha mashauri ya mauaji ambacho kimefanyika Mahakama ya mwanzo Makambako Hakimu mkazi mkuu mwenye mamlaka ya ziada Liadi Chamshama amesema washtakiwa hao walitenda kosa hilo Septemba 21, 2016.

Licha ya adhabu ya kutumikia miaka kumi jela, wametakiwa kumlipa Mama yao mdogo Rehema Ngimbudzi kila mmoja fedha kiasi cha shilingi milioni Tano.

Aidha Hakimu huyo wakati akisoma maelezo ya washtakiwa hao aliamuru mdhamini wa mshtakiwa namba moja bwana Christopher Joseph Salingwa kulipa faini ya shilingi milioni 4 au kwenda jela mwaka mmoja kwa kosa la kushindwa kumfikisha mshtakiwa mahakamani,ambapo shahidi huyo amelipa faini hiyo.

Awali mawakili wa washtakiwa hao, Happy Ilomo wakili wa mshtakiwa namba mbili Focus Lutengano na wakili Brighton kagua wakili wa mshtakiwa namba moja Aizack Lutengano waliomba Mahakama hiyo kuwapunguzia adhabu kwani wanategemewa na familia na ni mara yao ya kwanza kutenda kosa hilo.

Lakini hata hivyo wakili wa serikali Andrew Mandwa alimtaka hakimu kutoa adhabu kwa mujibu wa sheria ili iwe fundisho kwa wengine.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo