Bweni lawaka moto, Wanafunzi watatu wafariki dunia

Watoto watatu wa kike wenye ulemavu wa macho wamefariki Dunia kufuatia kutokea kwa ajali ya moto katika Bweni la kulelea watoto wenye ulemavu wa ngozi, uziwi na kutoona lililopo eneo la Buhangija Mkoani Shinyanga.


Taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP. Janeth Magomi imesema moto huo ulitokea majira yaa saa mbili na nusu usiku wa Novemba 23,, 2022 metokea jana Novemba 23,2022 katika bweni lililokuwa na watoto 32.


Amesema, “Polisi inafanya uchunguzi wa tukio la moto ambao chanzo chake bado hakijafahamika ulioteketeza bweni la kituo cha kulelea watoto walemavu Buhangija cha Shinyanga mjini na kusababisha vifo vya watoto wakike watatu.”


Kamanda Magomi amewataja waliofariki katika tukio hilo kuwa ni Caren Mayenga (10), Niliam Limbu (12) na Catherine Paulo (10) ambao ni Wanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya Msingi Buhangija.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo