Mama wa Marehemu Vumila Nassoro amesema tukio hilo lilitokea baada ya mwanae kumdai fedha shilingi 2000 mtuhumiwa na alipomuomba amrejeshee ndipo alikataa na kuibua mzozo uliosababisha mtuhumiwa kuchukua kisu kwenye pikipiki yake na kumchoma shingoni marehemu.
Mwenyekiti wa mtaa wa Mgulu wa ndege Veronika Michael ametbitisha kutokea tukio hilo ambapo amesema tukio hilo limetokea leo majira ya saa kumi na moja alfajiri katika kijiwe na pikipiki kilichopo katika mtaa huo wakati marehemu na mtuhumiwa wakitoka kwenye sherehe ya rafiki yao.