Pigo kwa Davido, ni baada ya mtoto wake kufariki dunia

Mtoto wa Davido, Ifeanyi Adeleke (3) amefariki dunia kwa kuzama kwenye bwawa la kuogelea (swimming pool) nyumbani kwao.


Vyombo mbalimbali vya habari Nigeria vimeripoti tukio hilo. Mapema Oktoba 31 Davido alionekana kumfundisha mtoto wake huyo kuogelea huku akimpongeza kwa kuimarika kwenye mchezo huo.


Taarifa zinasema Ifeanyi alizama kwenye maji kwa muda mrefu kabla ya wazazi wake kugundua kutokweka kwa mtoto wao. Baada ya kufanyika kwa msako walimkuta Ifeanyia akielea juu ya maji, na kumkimbiza hospitali lakini haikusaidia kuokoa maisha yake. 


Davido anakuwa msanii wa pili nchini Nigeria kumpoteza mtoto kwa kuzama kwenye maji hii ni baada ya kutokea kwa tukio kama hilo kwa msanii D'banji mnamo mwaka 2018.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo