Watoto wawili wamefariki kwa kuungua moto katika banda la kufugia kuku huku mwingine akijeruhiwa na moto huo ambao chanzo chake kikielezwa ni uchomaji takataka katika shimo la taka hizo.
Akizungumzia tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa ametaja majina ya watoto hao waliofariki kuwa ni Meshack Kyando (7) na Angrey Mgimba (2) huku mtoto aliyejeruhiwa na moto huo akifahamika kwa jina la Anold Mgimba.
