Daraja la Mto Kilombero labatizwa jina Daraja la Magufuli

Rais John Magufuli amezindua daraja la mto Kilombero ambalo kwa sasa linaitwa daraja la Magufuli.

Akitangaza jina la daraja hilo leo Mei 5 wakati Rais akizindua, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema ametoa jina hilo kutokana na juhudi alizozifanya Rais Magufuli wakati akiwa waziri wa ujenzi.

"Mheshimiwa Rais kwa mamlaka niliyopewa natangaza rasmi daraja hili litaitwa Magufuli, hii ni kutokana na juhudi kubwa uliyoiweka katika kufanikisha ujenzi wa daraja hili," amesema.

Daraja hilo lenye urefu wa zaidi ya mita 300 linaunganisha wilaya za Ulanga, Malinyi na Kilombero.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo