Wabunge wanaounda kambi ya Upinzani Bungeni wamesusia Bunge na kutoka nje ya Bunge hilo, wakati wakijadili bajeti ya Wizara ya mambo ya ndani ya nchi iliyowasilishwa Bungeni hapo na waziri mwenye dhamana, Mwigulu Nchemba.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, amesema wametoka nje kwa sababu ya kutoridhshwa na jinsi ambavyo Mwenyekiti wa Bunge anavyoendesha kikao hicho, kwani anawanyima uhuru wa kujadili masuala muhimu.
